Wednesday, October 31, 2012

KAULI YA MKUU WA MKOA DAR KUHUSU SILAHA ZINAZODAIWA KUFICHWA MISIKITINI.

                                       Maandamano ya oktoba 19/ 2012.
Kutokana na kuenea kwa taarifa kwamba katika baadhi ya Misikiti jijini Dar es salaam kumehifadhiwa silaha mbalimbali zinazotarajiwa kutumika kwenye maandamano ya waumini wa dini ya kiislamu watakaoandamana ijumaa novemba 2, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadick amesema Jeshi la polisi linazo taarifa na limejipanga.
Namkariri mkuu wa mkoa akisema “ninawataka wala siwaombi, waache utaratibu wao huo kama ni kweli hayo yanayoelezwa lakini nasema sisi kwa utaratibu wa kiserekali hatujapata hilo tishio lakini kama kuna mtu yeyote mwenye nia hiyo ya kuhamasisha watu waende na mapanga, anachezea moto… serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama vitakabiliana na hali yoyote na mtu yeyote atakaekuja na kitisho cha aina yoyote”
Mkuu huyo amesema maandamano hayo ambayo yanahamasishwa kupitia vipeperushi ambavyo vimetolewa na jumuiya na Taasisi za kiislam nchini ni batili hivyo polisi wamejipanga kwa atakaejitokeza.
Sadick amesema pia kwamba sababu zote zilizotolewa na jumuiya na taasisi hizo zimefanyiwa kazi ikiwemo ile ya kumchukulia hatua kijana anaedaiwa kudhalilisha kitabu cha dini hiyo pamoja na kukamatwa kwa watu wote waliohusika na vurugu zilizotokea katika baadhi ya maeneo Dar es salaam.
Maandamano ya sasa yamepangwa kufanyika ijumaa hii baada ya swala ya ijumaa Dar es salaam ambapo yamepangwa kuelekea kwenye ofisi ya Waziri mkuu na mikoani ni kwenye ofisi za Wakuu wa mikoa.

No comments:

Post a Comment