Thursday, October 18, 2012

Kwa kauli hii ya Ponda na Jumuiya za kiislamu kwa serikali watanzania tuseme nini?Je wameiweka serikali mikononi mwao na ni lazima ifanye kama wanavyotaka badala ya kufuata sheria na katiba ya nnchi.

  Waipa siku saba serikali kuwaachia watuhumiwa,waliochoma makanisa
JUMUIYA na Taasisi za Kiislamu nchini, zimeipa serikali siku saba kuwapa dhamana watuhumiwa wa Kiislamu wanaoshikiliwa kutokana na vurugu zilizotokea hivi karibuni maeneo ya Mbagala, jijini Dar es Salaam, na kusababisha makanisa kuchomwa moto na kuharibu mali nyingine kadhaa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika hoteli ya Lamada, Katibu wa Jumiya hiyo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema Waislam hao wanapaswa kupewa dhamana kwa kuwa ni haki yao kisheria.
Ponda alisema endapo siku hizo zitaisha bila kupewa haki hiyo watatangaza nini watakifanya ili kuondoa ukandamizaji huo.
Alisema katika vurugu zile waliokamatwa wengi ni Waislamu huku hoja ya kuwanyima dhamana ikiwa ni suala la kuharibiwa makanisa ambayo imechukuliwa kuwa ni ya kitaifa.
Tabia hiyo ya viongozi wa serikali kuyafanya mambo ya kanisa kuwa ya kitaifa na kudharau Waislamu na haki zao, Sheikh Ponda alisema ndiko kunakochangia kuligawa taifa katika misingi ya udini.
Sambamba na hilo pia waliitaka serikali kutoa tamko rasmi la kulaani kukojolea Kuran na kuongeza kwamba lile alilolitoa Rais Jakaya Kikwete katika kilele cha mbio za Mwenge hawalitambui na wala halitoshi kutokana na ukubwa wa tukio lenyewe.
Wasikitishwa JK kutotembelea misikiti
Jumuiya hiyo pia imesikitishwa na kitendo cha Rais kwenda kutembelea makanisa tu wakati vurugu hizo pia zilisababisha baadhi ya misikiti kuchomewa makapeti kwa mabomu yaliyokuwa yanarushwa na Jeshi la Polisi na watu kujeruhiwa.
“Rais alipofanya ziara katika kanisa la Zakiem alipita mita tatu jirani na msikiti wa Hijra ambapo makapeti yake mpaka tunakwenda mitamboni yameloa damu kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na polisi waliokuwa wakilinda doria katika kanisa hilo, alisema.
Waislamu hawajahusika na uvunjaji wa makanisa
Katika hatua nyingine Sheikh Ponda alisema Waislam hawajahusika na uvunjwaji wala uchomaji wa makanisa na kueleza vurugu zilitokea siku ambayo Waislam walikusanyika kwa wingi katika msikiti maalum kwa ajili ya ibada ya sala ya Ijumaa.
Alisema polisi walikuwa na upande katika tukio hilo kwani misikiti ya Ijumaa ilianza kuzingirwa mapema kuanzia majira ya saa 4:00 asubuhi na ilipofika majira ya saa 6:00 mchana baadhi ya misikiti ikiwemo ile iliyoko umbali wa kilometa mbili kutoka kituo cha polisi Maturubai, ilianza kushambuliwa kwa mabomu.
Wakati wa mashambulizi hayo, Ponda anadai makanisa yalionekana kupewa ulinzi wa amani huku misikiti ikipelekewa vikosi vya kushambuliwa.
Hata hivyo ilipotimu majira ya saa 9:00 alasiri alidai alifika mmoja wa maafisa kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ambaye aliwahoji masheikh waliokuwepo eneo la Maturabai na kutaka kujua ni kwa nini hawashiriki katika kusaidia kutuliza vurugu zinazoendelea kati ya polisi na Waislamu.
Baada ya kuwepo kwa mvutano wa muda mrefu kati ya Kamanda wa Polisi wa Temeke, Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Maturubai, masheikh hao na Waislamu waliofika kituo cha polisi cha Maturabai ili kushinikiza kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa aliyekojelea Kuran, muafaka ulikuwa ni masheikh kwenda viwanja vya Zakiem kwa lengo la kuwatuliza waumini wao.
Huku pendekezo la pili likiwa ni la Waislam wote waliokamatwa watolewe mahabusu na la tatu ni polisi kutoa gari na vipaza sauti kwa masheikh ambapo hilo la kuzungumza na waumini lilikamilika kwa msaada wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ambao walitoa msaada wa gari kwa masheikh.
“Kilichotokea baada ya masheikh kuondoka na waumini walijikuta wakishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kufanya vurugu ambapo polisi walimwagwa mitaani na kuwakamata watu wasiokuwa na hatia, ukamataji uliohusisha kuhojiwa watu majina, kuandamwa kwa mbio mtu aliyevaa kanzu, kofia na kuachwa aliyevaa msalaba akikatiza katikati ya askari na hatimaye matumizi ya nguvu kubwa kwa aliyekamatwa.
“Hatua hii ndiyo iliyopelekea kukamatwa kwa watuhumiwa wengi waliokuwa mikononi mwa polisi mpaka leo na ndiyo iliyochochea vurugu zilizosambaa mitaani,” alisema Sheikh Ponda.

No comments:

Post a Comment