Monday, January 13, 2014

MGOGORO WA WAKULIMA, WAFUGAJI KITETO:

Idadi ya waliofariki yakia kumi.

Miili ya watu waliofariki kutokana na mapigano ya kugombea ardhi baina ya wakulima na wafugaji katika hifadhi ya jamii ya Emboley Mortangosi wilayani Kiteto mkoani manyara, imeongezeka zaidi kutoka sita ilizopatikana juzi na kufikia jumla ya kumi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi Akili Mpwapwa amesema, nyumba zilizochomwa moto ni zaidi ya thelethini ambazo ni za wakulima.

Mapigano haya baina ya wakulima na wafugaji katika hifadhi ya jamii ya Emboly Mortangosi wilayani Kiteto kwa kipindi hiki, yametokea baada ya mkutano wa mkuu wa mkoa wa Manyara Elaston Mbwillo, alioufanya wiki iliyopita, kuwataka wakulima na wafugaji waliovamia hifadhi hiyo kuondoka ikiwa ni agizo la mahaka ya Rufaa.

Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi Akili Mpwapwa amesema, mapigano hayo yamezuka kwa wafugaji kuwashambulia wakulima na kuwaua pia kuchoma moto nyumba zao.

Mgogoro baina ya wakulima na wafugaji katika hifadhi ya Emboley Mortangosi wilayani Kiteto Mkoani Manyara, ulianza mwaka 2006 baada ya halmashauri ya wilaya hiyo, kuwaamuru wafugaji na wakulima waliovamia hifadhi kuondoka.

Wafugaji wamekuwa wakiwashambulia wakulima kwa kile kinachosemekana, wanadai wanastahili kuendelea kuishi katika hifadhi kwa kulisha mifugo yao ambayo haiharibu mazingira.

MWISHO

No comments:

Post a Comment