Wednesday, September 4, 2013

Arsenal wamevunja rekodi yao KATIKA USAJILI WA OZIL

Arsenal wamevunja rekodi yao kwa kumnasa Mmoja ya wachezaji bora Barani Ulaya, Mesut Ozil kutoka Real Madrid kwa pauni milioni 42.4 saa chache kabla dirisha la usajili kufungwa. 


Kiungo Mshambuliaji huyo kutoka ujerumani amepewa mkataba wa Miaka 5 na amemaliza kiu ya mashabiki wa Arsenal waliotaka mchezaji mwenye uwezo na jina kubwa kuletwa kwenye timu yao. Usajili wa Ozil umegharimu zaidi kuliko usajili wa mchezaji Dennis Bergkamp.

Ozili anategemewa kuongeza kasi ya ushambuliajina na kutengeneza mazingira mazuri ya Arsenal Kushinda Premier League.

Tottenham ndio klabu iliyotumia zaidi kwenye dirisha hili la usajili kwakutumia pauni milioni 105 kusajili wachezaji saba na kumpoteza Gareth Bale kwa Real  kwa pauni milioni 85.3

No comments:

Post a Comment