Monday, February 4, 2013

sherehe za miaka 36 ya CCM zafana sana mjini Kigoma,ccm wajigamba kwamba bado wanakubalika hata kwa wapinzani.










Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiingia uwanja wa Lake Tanganyika kuhitimisha sherehe za miaka 36 ya chama hicho mjini Kigoma leo

Ngoma za utamaduni zamfurahisha Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete

Akipungia kwa furaha maelfu ya wananchi wa Kigoma wanaomshangilia kwa nguvu

Licha ya vyombo kukorofisha msanii Diamond nma kundi lake walitumbuiza kwa ustadi

Diamond akipagawisha

Mwenyekiti wa CCM,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisisitiza jambo wakati wa hotuba yake kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma waliohudhuria Maadhimisho ya Miaka 36 ya kuzaliwa kwa CCM yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Mkoani Kigoma jioni hii.




Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akisema machache,muda mfupi kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa CCM,Rais Jakaya Mrisho Kikwete (hayupo pichani} kuwahutubia wananchi wa Mkoa wa Kigoma jioni hii.

Waziri wa Uchukuzi,Dkt. Harisson Mwakyembe akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Kigoma jioni hii na kuwahakikishia kuwa sasa hivi mkoa wa Kigoma mambo yako vyema kabisa na treni itaendelea kufanyaka kazi kama zamani.

Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi CCM,Nape Nnauye akiongoza shughuli hiyo.



Mwenyekiti wa CCM,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimia wananchi wa Mkoa wa Kigoma,wakati akiwasili kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika,kuongoza Maadhimisho ya 36 ya kuzaliwa kwa CCM,Mkoani Kigoma leo.


Mwenyekiti wa CCM,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia burudani ya ngoma.


Chipukizi wa CCM Mkoa wa Kigoma wakifanya Gwaride la heshima kwa Mwenyekiti wa CCM,Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Miaka 36 ya kuzaliwa kwa CCM,yaliyofanyika jioni hii kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma.


Mtangazaji mkongwe wa TBC Taifa Swedi Mwinyi akiwa hai hewani na wenzie
Katibu Mkuu wa CCM akiongea na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Omar Chambo na Maafisa waandamizi wa wakala wa usafiri wa anga
Washindi wa kombe la CCM 2013
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea banda la Uhuru na Mzalendo
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe Philip Mang'ula akipitia magazeti ya zamani kwenye banda la Uhuru na Mzalendo
Ankal akiwa na wanahabari wa Kigoma
Ngoma toka mkoa wa Makamba nchini Burundi
Wanahabari waliorekodi sherehe hizo kutoka vyombo mbalimbali
Mablogger wakirekebisha mitambo wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia. Kutoka shoto ni Ahmad, Othman, Bukuku, Nkoromo na Mroki


MUHIDIN MICHUZI at Sunday, February 03, 2013

No comments:

Post a Comment