WASHINGTON, Marekani
NCHI ya Marekani imepinga uamuzi wa Israel kujenga nyumba 3,000 za walowezi Mashariki mwa Jerusalem pamoja na Ukingo wa Magharibi kwa madai kuwa unarudisha nyuma jitihada za amani.
|  | 
| Hillary Clinton | 
NCHI ya Marekani imepinga uamuzi wa Israel kujenga nyumba 3,000 za walowezi Mashariki mwa Jerusalem pamoja na Ukingo wa Magharibi kwa madai kuwa unarudisha nyuma jitihada za amani.
Kwa mujibu wa Waziri wa nchi hiyo, Hillary Clinton
 alisema kuwa hatua hiyo itakuwa ikirudisha nyuma maendeleo ya nchi hiyo
 pamoja na jitihada ambazo zinafanywa katika kuleta amani.
"Naomba niseme  kwamba utawala huu, ni kama tawala
 zilizotangulia na umeweka bayana kwa Israel haiwezi kuendelea na ujenzi
 huo kwa kuwa  shughuli hizo zinarudisha nyuma jitihada za majadiliano 
ya amani," alisema Clinton.
Clinton alisema hayo  mbele ya hadhira alipokuwa 
akizungumza katika jukwaa lililoandaliwa na kituo cha sera za Mashariki 
iliyowajumuisha mawaziri  mbalimbali akiwemo Waziri wa Mambo ya Kigeni 
wa Israel, Avigdor Lieberman  pamoja na Waziri wa Ulinzi, Ehud Barak.
Pia Clinton alisema kuwa suluhisho la kudumu la 
mgogoro wa Gaza  lingekuwa  ni miongoni mwa  mipango mizuri ya kuleta 
amani  kati ya Israel na Wapalestina wote.
Utawala wa Rais Barack Obama ulijaribu kuzuia 
shinikizo la Palestina la kutambuliwa na Umoja wa Mataifa, kwa madai 
kuwa hatua hiyo imekuwa ni  kizingiti kikubwa  katika amani na kwamba 
taifa la Palestina lingetokana kwa kuwepo na mazungumzo na Israel.
Hata hivyo, Clinton alisema kuwa pande zote  mbili
 zinapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kutafuta njia ya kusonga mbele 
katika mazungumzo ambayo ndiyo yataleta suluhisho la mataifa mawili.
Aliongeza kuwa pande mbili zitakapokuwa tayari 
kushiriki katika  mazungumzo na Rais Obama  pia atakuwa tayari 
kushirikiana nao kikamilifu.
Kwa upande wa  msemaji wa Bazara la Taifa la 
Usalama, Tommy Vietor alisema kuwa vitendo hivyo haviwezi kuleta manufaa
 yoyote katika meza ya mazungumzo na kuongeza kuwa  Marekani inarejea 
upinzani wake wa muda mrefu dhidi ya makazi ya walowezi, pamoja na 
ujenzi Mashariki mwa Jerusalem.
"Tunaamini vitendo hivi havileti manufaa yoyote zaidi ya kuhujumu jitihada za kurudi kwenye meza ya mazungumzo," alisema Vietor.
"Tunaamini vitendo hivi havileti manufaa yoyote zaidi ya kuhujumu jitihada za kurudi kwenye meza ya mazungumzo," alisema Vietor.
Taarifa za vyombo vya habari zilisema kuwa  baadhi
 ya ujenzi wa Israel utafanyika katika eneo linalogombaniwa lililopo 
katika Ukingo wa Magharibi maarufu kama E1, ambalo linapita kati ya 
upande wa mwisho wa Mashariki ya eneo lililotekwa la Jerusalem 
mashariki, na makazi ya Maaleh Adumim.
Vilevile Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO), kimelaani hatua hiyo na kusema ni uvamizi dhidi ya taifa hilo.
Wapalestina wanapinga kwa nguvu zote, mradi wa E1 
kwa sababu unaligawanya eneo la Ukingo wa Magharibi katika vipande 
viwili - Kaskazini na Kusini, hatua ambayo inafanya uundwaji wa taifa la
 Palestina kuwa mgumu.
 
 
 
 

 
No comments:
Post a Comment