Sunday, November 11, 2012

Rais kikwete aweka jiwe la Msingi katika makao makuu mapya ya CCM Dodoma,Afungua mkutano mkuu wa nane


Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal,Rais wa Zanzibar,Dkt.Ali Mohamed Shein,Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Amana Abeid Karume 1pamoja na Makamu wa CCm Bara Pius Msekwa wakifunua kitambaa kuashiria kuweka jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa makao mapya ya CCM mjini Dodoma jana.
(Picha na Freddy Maro Ikulu)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa mkutano Mkuu wa nane wa Chama cha Mapinduzi wakati alipokuwa akiingia katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma jana.
Baadhi ya wajumbe wamkutano mkuu wa nane wa CCM wakati wa ufunguzi wa mkutano huo mjini Dodoma jana.
Baadhi ya wajumbe wamkutano mkuu wa nane wa CCM wakati wa ufunguzi wa mkutano huo mjini Dodoma jana.
Mwenyekiti wa CCM,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na kiongozi wa chama cha upinzani cha TLP Augustine Lyatonga Mrema wakati wa sherehe za ufunguzi wa mkutano mkuu wa nane wa CCM uliofanyika katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma jana.

Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake ya ufnugnuzi wakati wa mkutano Mkuu wa nane wa CCM katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma jana.Kushoto ni Makamu wa CCM Zanzibar Mhe.Amani Abeid Karume na kulia ni makamu mwenyekiti wa CCM Bara Mhe.Pius Msekwa

No comments:

Post a Comment