Friday, November 9, 2012

Hujuma kwa JK,wAENDESHA CAMPAIN CHAFU KUMTEMA UWENYEKITI

Katika kile kinachodaiwa kuwa ni kuhujuma dhidi ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, baadhi ya vipeperushi vimeonekana katika maeneo mbalimbali mjini hapa vikiwa na ujumbe unaosomeka: “CCM inayumba kwa pamoja tumpunguzie mzigo mheshimiwa Rais kwa kumvua  kofia moja ya uenyekiti, nina imani kwa pamoja tutashinda, piga kura ya hapana kwake, CCM oyeeee.”
Vipeperushi hivyo vimetawanywa mitaani na watu wasiojulikana tangu juzi.
Habari zaidi zinaeleza kuwa moja ya kundi ndani ya chama hicho, ndilo linalohusishwa na mkakati huo likidaiwa kwamba linataka Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar, Amani Karume apewe nafasi hiyo ili Rais Kikwete abaki na madaraka ya urais pekee.
Mmoja wa wajumbe wa mkutano huo, Agustino Matefu kutoka mkoani Morogoro alisema wamefuatilia na kubaini kuwa kuna makada wazito ndani ya chama hicho wanaohusika... “Hiki hapa kipeperushi mnaweza kukiona wenyewe,” alisema huku akionyesha.
Alisema mpango huo unasukwa na kundi ambalo linaongoza kwa kutoa rushwa katika chaguzi za chama hicho na kuandaa mtandao wa viongozi mbalimbali kwa lengo la kuwasaidia katika kampeni za urais.
Mjumbe huyo aliyekwenda mbali zaidi na kueleza kuwa Mtandao huo umetenga kiasi cha Sh5 bilioni kuwasaidia wagombea wao 10 katika nafasi za ujumbe wa Nec na kudai kwamba orodha ya wajumbe wao imekuwa ikipitishwa kwa wapiga kura kuwashawishi wawapigie kura nyingi.
Akizungumzia madai hayo, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa alisema hajaviona vipeperushi hivyo, lakini akasema kitendo hicho kimefanywa na watu wapuuzi ambao hawaijui CCM.
Alisema kitendo hicho hakijafanywa na wanaCCM wa Dodoma na kwamba watafanya kila linalowezekana kuwabaini watu hao.

Wakati wajumbe hao wakichuana kuwania nafasi hiyo kupitia kapu, uchaguzi wa Mjumbe wa Nec wilayani Longido, Arusha umebaki kitendawili.
Uchaguzi huo ulikwama mwezi uliopita baada ya wagombea kushindwa kufikisha nusu ya kura. Hao walikuwa Mbunge wa Loliondo, Lekule Laiser aliyepata kura 417, Peter Lemshau (381) na mwingine aliyeambulia kura 58.
Habari zilizopatikana jana zinasema mmoja wa wagombea yupo Dodoma kukutana na Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mkama kujua hatima ya uchaguzi huo.
Chanzo-Mwananchi

No comments:

Post a Comment