Monday, November 12, 2012

EXCLUSIVE: MANENO YA LORD EYEZ KUHUSU MASHABIKI WALIOPANGA KUMDHURU OMMY DIMPOZ, JINSI ALIVYOKAMATWA NA WALIOMTEKA.

0
Lord Eyez kwenye exclusive interview na Lord Eyez..
Lord Eyez wa N2N Soldiers amefanya Exclusive interview na millardayo.com na kuzungumza ishu kadhaa kuhusu tuhuma za wizi wa vifaa vya gari la Ommy Dimpoz.
Kwanza alianza kwa kuzungumza na wale mashabiki zake waliotoa vitisho vya kumdhuru Ommy Dimpoz huku wengine wakimwambia asikanyage Arusha na hiyo yote ni kutokana na kukasirishwa na kitendo cha Ommy Dimpoz kusambaza picha za Lord Eyez na kumuita mwizi.
Namkariri Eyez akisema “mi ninachosema wasimuhukumu mtu kwanza wala wasipandwe, wanahitaji kujua ukweli na wasifanye matukio yoyote ambayo ni ya uvunjaji wa sheria na pia wachague marafiki, wawe wastaarabu, wawe wapole na wawe na subira… wasimjengee chuki binadamu, mi mwenyewe nimekua mtu wa kusamehe sana ndio maana nakwambia wamwachie Mungu, kwa kuwa mimi sina chuki na mtu siwezi kumshauri mtu awe na chuki na mtu lakini malipo ni hapahapa duniani na Mungu yupo wamwamini sana sababu ndio anafanya kila kitu”
.
Jinsi alivyokamatwa siku ya tukio, Lord Eyez amesema alipigiwa simu na mwanaume alafu baadae akaongea na mwanamke ambae alitaka waonane Kinondoni mida hiyo ambapo alikwenda kwenye eneo la tukio bila kujua kitatokea nini.
Alipofika zilikuja gari 3 zenye watu wengi ikabidi ahamaki, wakaanza kama kumzingua na jamaa mmoja akasikika akisema huyu atatusaidia kumpata tunaemtafuta, walimshikilia Lord Eyez kwa masaa yasiyopungua manne kwa mujibu wa maelezo ya Wakili wake.

.
Wakati wamemshikilia Lord Eyez akasema huyo jamaa wanaedhani ni mshkaji wake ambae ndio anadaiwa kuhusika na wizi wamejuana hazipiti hata wiki mbili na hamjui kihivyo, baada ya hapo walimchukua mpaka kwenye eneo lilipo gari la Ommy Dimpoz lililoibiwa vifaa ambapo Eyez anasema walipofika kwenye hilo gari, kweli alishuka ili aliangalie kwa sababu alikua anashangaa pia lakini akapigwa picha ambazo baadae ndio zilisambazwa kwamba ni ushahidi wa wizi aliofanya.
Eyez amesema watu hao waliomshikilia kwa saa kadhaa walitaka kumzingua na kumpiga lakini kiongozi wao alizuia mtu asimguse.
Amesema hii ni mara yake ya kwanza kushikiliwa na polisi ambapo hii ya juzi alishikiliwa kwa zaidi ya siku kumi na mbili na anasisitiza kwamba sio kweli yeye ni mwizi, hawezi kuifanyia jamii mambo kama hayo.
Kuna mengine aliyoyaongea Lord Eyez ambayo ni Exclusive on millardayo.com na AMPLIFAYA ya CLOUDS FM, utaendelea kuyasoma na kuyasikia siku baada ya siku.
facebook.com/millardayo twitter.com/millardayo

No comments:

Post a Comment